Psalms 16

Sala Ya Matumaini

(Utenzi wa Daudi)


1 aEe Mungu, uniweke salama,
kwa maana kwako nimekimbilia.


2 bNilimwambia Bwana, “Wewe ndiwe Bwana wangu;
pasipo wewe sina jambo jema.”

3 cKwa habari ya watakatifu walioko duniani,
ndio walio wa fahari ambao ninapendezwa nao.

4 dHuzuni itaongezeka kwa wale
wanaokimbilia miungu mingine.
Sitazimimina sadaka zao za damu
au kutaja majina yao midomoni mwangu.


5 e Bwana umeniwekea fungu langu na kikombe changu;
umeyafanya mambo yangu yote yawe salama.

6 fAlama za mipaka zimeniangukia mahali pazuri,
hakika nimepata urithi mzuri.


7 gNitamsifu Bwana ambaye hunishauri,
hata wakati wa usiku moyo wangu hunifundisha.

8 h iNimemweka Bwana mbele yangu daima.
Kwa sababu yuko mkono wangu wa kuume,
sitatikisika.


9 jKwa hiyo moyo wangu unafurahia, na ulimi wangu unashangilia;
mwili wangu nao utapumzika salama,

10 kkwa maana hutaniacha kaburini,
wala hutamwacha Mtakatifu Wako kuona uharibifu.

11 lUmenijulisha njia ya uzima;
utanijaza na furaha mbele zako,
pamoja na furaha za milele
katika mkono wako wa kuume.
Copyright information for SwhKC